Page 42 - SayansiStd4
P. 42

Namna ya kuzuia tetekuwanga

              Tetekuwanga huzuiwa kwa kutochangia mavazi na kuzingatia
              usafi wa mwili na mavazi kwa mgonjwa. Vilevile, dawa ya kuua
              vimelea vya magonjwa itumike wakati wa kusafisha mwili na
          FOR ONLINE READING ONLY
              kufua nguo. Aidha, tetekuwanga huzuiwa kwa chanjo.




               Zoezi namba 4
               1.  Eleza namna  ambavyo  tetekuwanga  inaweza  kuenea

                     kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine.

               2.  Unawezaje kutambua kama mtu ana tetekuwanga?


               3.  Ni mambo gani unaweza kufanya ili kuzuia kuenea kwa
                     tetekuwanga?




              Kifua kikuu

              Ugonjwa wa kifua kikuu unasababishwa na bakteria. Ugonjwa
              huu  unaathiri  zaidi  mapafu. Hata hivyo, unaweza  kuathiri
              sehemu zingine za mwili kama vile uti wa mgongo, mifupa na

              figo. Ugonjwa wa kifua kikuu huenezwa kwa njia ya hewa, hasa
              mtu aliye na vimelea vya kifua kikuu akikohoa au kupiga chafya.
              Pia, kutema mate ovyo husababisha vijidudu kusambaa. Hali

              hii husababisha mtu mwingine kuambukizwa.

              Dalili za kifua kikuu

              Zifuatazo ni miongoni mwa dalili za ugonjwa wa kifua kikuu:


              (a)  Kukohoa mfululizo kwa muda wa wiki mbili au zaidi;

              (b)  Kupata maumivu ya kifua;

              (c)  Homa za usiku na kutoka jasho jingi usiku;


              (d)  Kupungua uzito ndani ya muda mfupi;



                                                   35




                                                                                            14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   35
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   35                                   14/01/2025   18:39
   37   38   39   40   41   42   43   44   45   46   47