Page 43 - SayansiStd4
P. 43

(e)  Kukohoa damu; na

              (f)  Kukosa hamu ya kula chakula.

              Namna ya kuzuia kifua kikuu
          FOR ONLINE READING ONLY
              Kifua kikuu hudhibitiwa kwa njia ya chanjo kwa watoto wachanga.

              Njia nyingine za kuzuia ni pamoja na kuzingatia usafi wa mwili,
              kuepuka msongamano wa watu. Pia, epuka kuchangia vyombo
              na watu wenye maambukizi. Watu waliopata maambukizi ya
              kifua kikuu hupatiwa dawa  za kutibu  ugonjwa  huo  chini  ya
              uangalizi wa mhudumu wa afya.



               Zoezi namba 5

               1.  Eleza namna kukohoa, kupiga chafya, na kutema mate
                     kunavyoweza kuchangia kuenea kwa kifua kikuu.


               2.  Dalili  gani  zinaweza  kukuwezesha  kumtambua  mtu
                     mwenye kifua kikuu?

               3.  Ni sehemu  gani  nyingine  za mwili  ambazo  kifua kikuu

                     kinaweza kuathiri mbali na mapafu?


              Virusi vya UKIMWI (VVU) na UKIMWI
              UKIMWI husababishwa na Virusi vya UKIMWI (VVU). VVU

              hushambulia  chembe hai  nyeupe  za damu ambazo  hujenga
              kinga ya mwili. Chembe hai hizo zinaposhambuliwa na VVU
              husababisha mwili kupoteza uwezo wa kujikinga dhidi ya vimelea
              vya magonjwa.  Virusi vya UKIMWI  vinapozidi  kuongezeka

              hudhoofisha mwili na kusababisha kushambuliwa na magonjwa.
              Udhaifu wa mwili na magonjwa huweza kusababisha kifo.














                                                   36



                                                                                            14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   36
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   36                                   14/01/2025   18:39
   38   39   40   41   42   43   44   45   46   47   48