Page 45 - SayansiStd4
P. 45

FOR ONLINE READING ONLY





















                    Kielelezo namba 5: Mgonjwa anayeongezewa damu salama


              (c)  Maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.  Mtoto
                   anaweza kupata VVU kutoka kwa mama anayeishi na
                   VVU hasa wakati wa kujifungua. Vilevile, mtoto anaweza

                   kupata VVU kutoka kwa mama anayeishi na VVU wakati
                   wa kunyonya.

              (d)  Kufanya ngono na mtu mwenye VVU. Watoto hawatakiwi
                   kujihusisha  na vitendo  vya ngono.  Vilevile,  wasipite  na

                   kucheza maeneo hatarishi yenye vishawishi vya kubakwa.
                   Maeneo hayo ni kama vile vilabu vya pombe na kumbi za
                   starehe. Maeneo mengine ni kama vile magofu ya nyumba
                   na vibanda  vya kuoneshea  sinema.  Aidha, ni muhimu
                   kutoa taarifa kwa wazazi au walimu mapema endapo mtu

                   yeyote ataonesha dalili za kutaka kukufanyia vitendo vya
                   ngono ili kupata msaada sahihi.

              Namna ya kuzuia maambukizi ya VVU na UKIMWI

              VVU ni hatari na havina chanjo wala tiba. Hata hivyo, mtu





                                                   38



                                                                                            14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   38
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   38                                   14/01/2025   18:39
   40   41   42   43   44   45   46   47   48   49   50