Page 44 - SayansiStd4
P. 44

Njia za maambukizi ya VVU

              VVU vinakaa kwenye majimaji ya mwili wa binadamu hasa
              damu. VVU huambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa
              mwingine kwa njia mbalimbali kama vile zifuatazo:
          FOR ONLINE READING ONLY

              (a)  Kuchangia  mswaki  na vifaa vyenye  ncha  kali  kama
                   sindano, wembe, hereni, pini na mkasi. Kuchangia
                   vifaa vyenye ncha kali na mtu  mwenye VVU kunaweza

                   kusababisha maambukizi. Kielelezo namba 4 kinaonesha
                   vifaa vinavyoweza kuchangia maambukizi ya VVU.




























               Kielelezo namba 4: Vifaa vinavyoweza kuchangia maambukizi ya VVU


              (b)  Kuongezewa damu yenye VVU. Kuongezewa damu yenye
                   VVU kunasababisha maambukizi. Damu ni lazima ipimwe
                   na kuhakikiwa kuwa ipo salama na kuwa haina VVU kabla

                   ya kumwongezea mgonjwa. Kielelezo namba 5 kinaonesha
                   mgonjwa anayeongezewa damu salama katika kituo cha
                   afya.










                                                   37




                                                                                            14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   37
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   37                                   14/01/2025   18:39
   39   40   41   42   43   44   45   46   47   48   49