Page 49 - SayansiStd4
P. 49

kusababishwa na mazingira. Mzio unaotokana na baadhi ya
              vitu katika mazingira huchochea pumu kuanza. Vitu hivyo ni
              kama vile moshi, vumbi, harufu ya manukato au sabuni  na
              chavua za maua. Vitu hivyo husababisha kuvimba na kujaa ute
          FOR ONLINE READING ONLY
              mzito katika kuta za ndani za njia ya hewa. Hali hii inapotokea
              huzifanya njia hizo kuwa nyembamba. Njia za kupitisha
              hewa  zinapokuwa  nyembamba  hupunguza kiasi  cha hewa
              kinachoingia na kutoka na kufanya pumzi kubana.


              Dalili za pumu

              Dalili za ugonjwa wa pumu ni kama zifuatazo:


              (a)  Kukohoa, kupiga chafya na mafua;

              (b)  Kubanwa na kuumwa kifua na mbavu; na

              (c)  Pumzi kubana kunakoambatana na sauti kama filimbi au

                   mluzi.

              Namna ya kuzuia pumu

              Pumu ni hali ya  kudumu ambayo haina  tiba. Ugonjwa huu
              unaweza kuzuiwa kwa:


              (a)  Kuepuka vichochezi vya pumu mfano chavua na manukato;
                   na

              (b)  Kupata matibabu ya kutuliza pumu mapema pindi dalili za

                   awali zinapojitokeza.





















                                                   42



                                                                                            14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   42                                   14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   42
   44   45   46   47   48   49   50   51   52   53   54