Page 48 - SayansiStd4
P. 48

Dalili za kisukari

              Zifuatazo ni miongoni mwa dalili za kisukari:

              (a)  Kukojoa mara kwa mara;
          FOR ONLINE READING ONLY
              (b)  Kupungua uzito kwa haraka;

              (c)  Kuwa na kiu isiyoisha hata kama utakunywa maji ya
                   kutosha;

              (d)  Uchovu wa mwili;


              (e)  Kutoona vizuri;

              (f)  Vidonda visivyopona haraka; na

              (g)  Kupata ganzi mikononi au miguuni.


              Namna ya kuzuia kisukari

              Ugonjwa wa kisukari unaweza kudhibitiwa kwa kufuata kanuni
              za afya bora. Kanuni hizo ni pamoja na ulaji sahihi na kudhibiti
              ongezeko la uzito wa mwili. Tunashauriwa kufanya mazoezi ya

              mwili mara kwa mara ili kupunguza hatari ya kupata kisukari.

               Zoezi namba 7
               1.  Taja  dalili  tatu zinazokuwezesha  kutambua kuwa  mtu

                     ana ugonjwa wa kisukari.

               2.  Kwa nini mazoezi ya mwili ya mara kwa mara yanaweza

                     kusaidia kuzuia ugonjwa wa kisukari?

               3.  Eleza kwa nini ulaji sahihi wa vyakula unaweza kuzuia

                     ugonjwa wa kisukari.



              Pumu

              Pumu ni aina ya ugonjwa unaoathiri  mfumo  wa upumuaji.
              Ugonjwa wa pumu unaweza kurithiwa kutoka kwa wazazi au



                                                   41




                                                                                            14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   41                                   14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   41
   43   44   45   46   47   48   49   50   51   52   53