Page 70 - SayansiStd4
P. 70

5.  Maji yakipata joto huchemka na kubadilika kuwa _____.


                     (a)  mvuke

                     (b)  maziwa
          FOR ONLINE READING ONLY
                     (c)  barafu
                     (d)  kimiminika


               Sehemu B:  Andika KWELI kwa sentensi sahihi na SI KWELI
                               kwa sentensi isiyo sahihi.

               6.  Maji yaliyopatikana kwa kupoza mvuke wa maji ni safi
                     na salama.


               7.  Mara nyingi mvua ya mawe hutokea katika mazingira
                     yenye jotoridi la chini sana.

               8.  Maji yaliyochemshwa na kufikia kizingiti cha mchemko

                     wa maji ni salama kwa kunywa.

               9.  Chakula kilichogandishwa kinaweza kudumu kwa muda

                     mrefu bila kuharibika.

               10.  Wakati maji yanaganda, hubadirika  kuwa gesi mara

                     moja.

               Sehemu C: Maswali ya majibu mafupi


               11.  Eleza namna unavyoweza kubadili maji kuwa mvuke na
                     kutoka mvuke kurudi katika hali ya kimiminika (maji).

               12.  Unawezaje  kutumia maji yakiwa katika hali ya yabisi,

                     kimiminika na gesi?

               13.  Eleza umuhimu wa kizingiti cha mgando wa maji na
                     kizingiti cha mchemko wa maji.


               14.  Tofautisha sifa ya maji katika hali yabisi, kimiminika na
                      gesi.


                                                   63




                                                                                            14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   63                                   14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   63
   65   66   67   68   69   70   71   72   73   74   75