Page 80 - SayansiStd4
P. 80
Hasara za kuungua kwa vitu
Uunguaji wa vitu huweza kusababisha hasara mbalimbali.
Miongoni wa hasara hizo ni:
FOR ONLINE READING ONLY
(a) Uharibifu mkubwa wa mazingira kwa kuharibu uoto wa
asili na makazi ya wanyama;
(b) Mmomonyoko wa udongo na kupoteza rutuba ya ardhi
Uchomaji wa misitu unaweza kusababisha;
(c) Kuharibu majengo na vifaa mbalimbali vyenye thamani, na
kusababisha upotevu mkubwa wa mali. Kielelezo namba 4
kinaonesha uunguaji wa vitu; na
Kielelezo namba 4: Uunguaji wa vitu
(d) Kuungua kwa vitu kama vile mkaa na mafuta ya petroli,
huchangia ongezeko la gesi chafuzi angani.
Kujilinda na kuungua
Kujilinda dhidi ya ajali zinazohusisha vitu vinavyoungua,
kunahitaji mbinu mbalimbali za kimaandalizi na kiusalama.
Zifuatazo ni mbinu ambazo zitakulinda wewe na wengine dhidi
ya ajali zinazosababishwa na vitu vinavyoungua:
Hifadhi vizuri vifaa vinavyolipuka
Weka mbali na vyanzo vya joto na moto vitu vinavyoweza
kulipuka (kama petroli, mafuta ya taa na kemikali);
73
14/01/2025 18:39
SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd 73 14/01/2025 18:39
SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd 73