Page 26 - Jiografia_Mazingira
P. 26

Sura

                  ya                  Pande Kuu za Dunia


                 Pili
        FOR ONLINE READING ONLY





             Utangulizi


            Binadamu  anapotembea  hufuata uelekeo fulani wa dunia  ili
            kufika sehemu aliyokusudia. Ili kubaini uelekeo sahihi, Pande

            Kuu  za  Dunia  hutumika.  Kijiografia  yapo  majina  maalumu
            ambayo hutumika kubainisha Pande Kuu za Dunia. Katika sura
            hii utajifunza kuhusu maana ya Pande Kuu za Dunia, kuchora,

            na kubaini Pande Kuu za Dunia. Pia, utajifunza  kuhusu pande
            nane za dunia na umuhimu wa kutumia Pande Kuu za Dunia.
            Umahiri  utakaoujenga  utakuwezesha  kutumia  Pande  Kuu  na
            pande nane za Dunia  kubaini mahali na uelekeo.






                         Fikiri
                       Namna ya kubaini njia kwa kutumia Pande Kuu za

                       Dunia

          Maana ya Pande Kuu za Dunia

          Pande Kuu za Dunia ni alama za msingi za mwongozo zinazotumika
          kuonesha uelekeo wa sehemu tofauti za dunia. Uelekeo huo ni Kaskazini,
          Kusini, Mashariki na Magharibi. Kila uelekeo unawakilisha upande

          fulani wa dunia. Mara nyingi, Pande Kuu za Dunia zinapoandikwa
          huwakilishwa kwa herufi. Kwa mfano, Kaskazini huwakilishwa
          na herufi (Kas), Kusini  huwakilishwa na herufi (Kus), Mashariki
          huwakilishwa na herufi (Mas), na Magharibi huwakilishwa na herufi

          (Magh). Alama za Pande Kuu za Dunia mara nyingi huoneshwa




                                                 19



                                                                                          31/10/2024   19:18
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   19
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   19                                           31/10/2024   19:18
   21   22   23   24   25   26   27   28   29   30   31