Page 29 - Jiografia_Mazingira
P. 29

Njia za kubaini Pande Kuu za Dunia

          Pande Kuu za Dunia zinaweza kubainishwa kwa kutumia njia
          mbalimbali. Njia hizi ni kwa kutumia  mawio na machweo ya Jua,
          uelekeo wa kivuli, uelekeo wa nyota, kwa kutumia ramani, na kwa
          kutumia dira. Katika hatua hii tutajifunza kubaini Pande Kuu za
        FOR ONLINE READING ONLY
          Dunia kwa kutumia mawio na machweo ya Jua, uelekeo wa kivuli,
          ramani, na dira.


          Kubaini Pande Kuu za Dunia kwa kutumia mawio na machweo

          ya Jua

          Kuangalia Jua linapochomoza wakati wa asubuhi au linapozama
          wakati wa jioni ni njia mojawapo ya kubaini Pande Kuu za Dunia
          katika eneo ulilopo. Kwa kawaida, Jua huchomoza upande wa
          Mashariki na kuzama upande wa Magharibi. Kitendo hiki cha asili

          hurahisisha kutambua upande wa Mashariki na Magharibi wa mahali
          ulipo. Kwa kutambua uelekeo wa mawio na machweo, unaweza
          kukuza uelewa wa msingi wa Pande Kuu za Dunia.

          Hivyo, wakati wa asubuhi, ukisimama kwa kulitazama Jua upande
          huo ni Mashariki, na Magharibi ni upande ulikoelekeza mgongo.

          Upande wa kulia utakuwa ni Kusini na upande wa kushoto ni
          Kaskazini. Vivyohivyo, wakati wa jioni ukilitazama jua linapozama
          upande huo ni Magharibi, wakati nyuma yako kutakuwa ni Mashariki,
          kulia kwako ni Kaskazini na kushoto kwako ni Kusini.

          Kubaini Pande Kuu za Dunia kwa kutumia uelekeo wa kivuli

          Uelekeo wa kivuli chako wakati wa asubuhi na jioni unaweza kutumika
          kubaini Pande Kuu za Dunia. Kwa kawaida, unapotembea wakati

          wa asubuhi upande ambao kivuli chako kilipo ndio Magharibi. Kwa
          mfano, ukitembea kwa kulitaza Jua, kivuli chako kitakuwa nyuma
          yako, na ikiwa utatembea kwa kuligeuzia Jua mgongo, kivuli chako

          kitakuwa mbele yako, hivyo, upande huo ni Magharibi. Vilevile,
          wakati wa jioni, upande ambao kivuli chako kilipo ndio Mashariki
          yako, kama inavyoonekana katika Kielelezo namba 2.





                                                 22



                                                                                          31/10/2024   19:18
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   22                                           31/10/2024   19:18
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   22
   24   25   26   27   28   29   30   31   32   33   34