Page 31 - Jiografia_Mazingira
P. 31

2.  Mwalimu wako akiwa ametazama upande wa Kaskazini,
                 kushoto kwake kutakuwa ni upande gani?

              3.  Kama umepotea msituni na ukabaini Jua linazama upande
                 wako wa kulia,  je, wewe utakuwa umetazama upande gani?
        FOR ONLINE READING ONLY
              4.  Unapotembea wakati wa jioni, endapo kivuli chako kitakuwa
                 mbele yako, je utakuwa unaelekea upande gani?



          Kubaini Pande Kuu za Dunia kwa kutumia ramani

          Ramani ni mwongozo mmojawapo unaotumika kubaini Pande Kuu
          za Dunia. Miongoni mwa vipengele muhimu vya ramani ni alama
          ya  uelekeo wa Kaskazini. Matumizi ya alama hii katika ramani ni

          kurahisisha kubaini Pande Kuu za Dunia yaani: Kaskazini, Kusini,
          Mashariki na Magharibi.

                     Kazi ya kufanya namba 3

                       Chunguza Kielelezo namba 3 kisha; bainisha uelekeo wa
                   vitu kulingana na maelekezo uliyopewa;

































                                Kielelezo namba  3: Mtaa wa ziwani





                                                 24



                                                                                          31/10/2024   19:18
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   24
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   24                                           31/10/2024   19:18
   26   27   28   29   30   31   32   33   34   35   36