Page 32 - Jiografia_Mazingira
P. 32

Maswali

             (a) Bainisha uelekeo wa kituo cha bajaji kwa kutokea eneo la

                kambi.

             (b) Fikiri, upo eneo yalipo makazi na unataka kwenda kivukoni,
        FOR ONLINE READING ONLY
                je, utafuata uelekeo gani?

             (c) Ziwa lipo upande gani wa makazi?

             (d) Kanisa lipo upande gani wa eneo la kambi?

             (e) Msikiti upo upande gani wa viwanja vya michezo?

          Kubaini Pande Kuu za Dunia kwa kutumia dira


          Dira ni kifaa kinachotumiwa kutambua uelekeo wa Kaskazini. Zipo
          aina mbili za dira, ambazo ni; dira ya kidijitali na dira ya analojia.
          Dira ya kidijitali hutumia teknolojia kusoma na kuonesha uelekeo
          wa Kaskazini. Aina hii ya dira imeunganishwa kwenye GPS, saa
          za kisasa, simujanja na vyombo vya usafiri kama vile magari, boti

          na ndege kama inavyoonekana katika Kielelezo namba 4. Dira ya
          analojia hutumia vipande vya sumaku au sindano yenye sumaku
          kuelekeza upande wa  Kaskazini.





























                               Kielelezo namba 4: Dira ya kidijitali





                                                 25



                                                                                          31/10/2024   19:18
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   25
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   25                                           31/10/2024   19:18
   27   28   29   30   31   32   33   34   35   36   37