Page 34 - Jiografia_Mazingira
P. 34

(c)  chora mstari mwingine ulionyooka katikati ya upande wa Kusini
               na upande wa Mashariki, ukianzia pale mistari ya pande hizo
               ilipokutana, kisha andika Kusini-Mashariki ( Kus-Mas);

          (d) chora mstari mwingine ulionyooka katikati ya upande wa Kusini
               na upande wa Magharibi, ukianzia pale mistari ya pande hizo
        FOR ONLINE READING ONLY
               ilipokutana kisha andika Kusini-Magharibi (Kus-Magh); na

          (e) chora mstari mwingine ulionyooka katikati ya upande wa Kaskazini
               na upande wa Magharibi, ukianzia pale mistari ya pande hizo
               ilipokutana, kisha andika Kaskazini-Magharibi (Kas-Magh).

          Baada ya kuchora mchoro wako, bila shaka umepata pande nane

          za dunia.
          Zingatia: Unaposoma au unapoonesha pande nane za dunia, unapaswa

          kuanzia upande wa Kaskazini au Kusini. Hii ni kwa sababu pande
          hizi ni alama za msingi katika dira zinazotumika katika uelekezaji.
          Pia, alama hizi ndio msingi wa kukuongoza kutambua pande nane
          za dunia, kama inavyoonekana katika Kielelezo namba 5.




































                            Kielelezo namba 5: Pande nane za dunia




                                                 27



                                                                                          31/10/2024   19:18
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   27                                           31/10/2024   19:18
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   27
   29   30   31   32   33   34   35   36   37   38   39