Page 47 - Jiografia_Mazingira
P. 47

Kuchora ramani sahili ya shule
          Ramani ya shule ni mchoro unaoonesha muundo wa shule, kama vile

          viwanja vya michezo, majengo yakiwemo;  vyumba vya madarasa,
          ofisi za waalimu, na maeneo mengine muhimu. Hatua zifuatazo
          zitakuwezesha kuchora ramani ya shule:
        FOR ONLINE READING ONLY
            (a) Tambua ukubwa, umbo na uelekeo wa eneo la shule;

            (b) bainisha ukubwa, maumbo na mahali vilipo vitu muhimu katika
               eneo la shule;

            (c) andaa eneo litakalotumika kuchora ramani ya shule, kwa kuchora
               umbo la mraba au mstatili kwenye karatasi. Hakikisha umeacha
               eneo kwa ajili ya kichwa cha ramani, ufunguo na maelezo; na

            (d) fuata hatua za uchoraji wa ramani sahili kuchora ramani ya
               shule.

                     Kazi ya kufanya namba 4

                          Chora ramani sahili kuonesha mazingira ya shule yako
                 kwa kuzingatia hatua za uchoraji wa ramani ya shule.


                       Zoezi la pili



              1.  Ni vifaa gani muhimu unapaswa kuviandaa unapotaka
                 kuchora ramani?

              2.  Chora alama zinazotumika kuwakilisha vitu vifuatavyo:
                 (a) Majengo;

                 (b) miti;

                 (c) barabara;

                 (d) msikiti;

                 (e) kanisa; na
                 (f) daraja.

              3.  Eleza tofauti ya ramani ya darasa na ramani ya shule.

              4.  Eleza kazi ya ufunguo katika ramani.





                                                 40



                                                                                          31/10/2024   19:18
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   40
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   40                                           31/10/2024   19:18
   42   43   44   45   46   47   48   49   50   51   52