Page 49 - Jiografia_Mazingira
P. 49
Maswali
1. Bainisha vitu vinavyoonekana katika ramani ya Kata ya Sinza.
2. Bainisha vipengele muhimu vya ramani vilivyozingatiwa
katika ramani hiyo.
FOR ONLINE READING ONLY
3. Chora ramani ya Kata ya Sinza, kisha onesha vitu vifuatavyo:
(a) Barabara iliyopo Kusini Magharibi mwa ramani;
(b) Msikiti uliopo Kusini mwa ramani;
(c) Kata iliyopo Kaskazini mwa ramani;
(d) Mto uliopo Kusini mwa ramani;
(e) Hospitali iliyopo kusini Magharibi mwa Kijitonyama; na
(f) Ofisi iliyopo Kusini mwa Barabara ya Mlandizi.
Kuchora ramani ya wilaya
Wilaya ni mgawanyiko wa kiutawala wa eneo fulani ndani ya nchi.
Wilaya hujumuisha kata au tarafa kadhaa. Kila wilaya inaongozwa
na mkuu wa wilaya ambaye huteuliwa na rais.
Kazi ya kufanya namba 6
Chunguza Kielelezo namba 6 kisha jibu maswali yanayofuata:
Kielelezo namba 6: Mkoa wa Dodoma
42
31/10/2024 19:18
JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd 42 31/10/2024 19:18
JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd 42