Page 52 - Jiografia_Mazingira
P. 52

Mambo ya kuzingatia
          Uchoraji wa ramani kidijitali kwa kutumia programu ya “Google My

          Maps” unazingatia mambo yafuatayo;

          (a) Uwepo wa simujanja, tabuleti au kompyuta;
        FOR ONLINE READING ONLY
          (b) hakikisha kifaa kimeunganishwa na mtandao;
          (c) tambua eneo la kijiografia unalotaka kuchora katika ramani,

              mfano mipaka ya nchi, barabara au ziwa; na

          (d) hakikisha una akaunti katika tovuti ya Google kwa kujisajili
              kwanza. Tumia anuani ya “Google My Maps” katika kujisajili.
              Anuani hii itakuruhusu kuunda ramani mwenyewe kwa kuchora
              maumbo na kuweka alama za vitu mbalimbali.


          Hatua za uchoraji wa ramani kwa kutumia programu ya ‘Google
          My Maps’
          Zifuatazo ni hatua za kufuata unapochora ramani kwa kutumia
          programu ya “Google My Maps.” Ramani ya hifadhi ya Wanyama

          ya Swaga Swaga iliyopo mkoa wa Dodoma imetumika kama mfano.

            1.  Tumia kivinjari chako, ingia katika tovuti ya ‘Google’ kisha andika
               ‘Google My Maps’ kama inavyoonekana katika Kielelezo namba
               7, kisha bofya sehemu imeandikwa “My Maps”




























                             Kielelezo namba. 7: Kivinjari cha wavuti



                                                 45



                                                                                          31/10/2024   19:18
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   45
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   45                                           31/10/2024   19:18
   47   48   49   50   51   52   53   54   55   56   57