Page 72 - Jiografia_Mazingira
P. 72

Maswali


           Kwa kutumia rula;

               (a) Kokotoa umbali wa kutoka Kitunda Misioni mpaka ofisi ya
                   kijiji.
        FOR ONLINE READING ONLY
               (b) Kokotoa umbali wa kutoka ofisi ya kijiji mpaka ofisi ya
                   kitongoji.

               (c) Kokotoa umbali wa kutoka ofisi ya kitongoji mpaka Kitunda
                   Misioni.


          Upimaji wa umbali usionyooka


          Ili kupima umbali wa vitu visivyonyooka kama vile mto, barabara au
          reli, vifaa kama bikari, kipande cha karatasi, uzi na skeli ya ramani
          hutumika.

            1.  Kutumia uzi

          Zifuatazo ni hatua za kubaini umbali usionyooka katika ramani kwa
          kutumia uzi.

              (a) Baini vituo viwili vinavyounganika kwa mstari usionyooka.
                  Kwa mfano, kituo A na B, kisha gawa umbali unaohitajika

                  kupimwa katika vipande vifupivifupi ambavyo vimenyooka na
                  weka alama kama inavyoonekana katika Kielelezo namba 13.











          Kielelezo namba 13: Umbali unaohitajika kupimwa kutoka kituo A hadi kituo B
              (b) Chukua uzi na ufunge fundo kwenye ncha ya mwisho upande

                  wa kushoto, kisha ulaze uzi huo kwenye mstari usionyooka
                  unaounganisha vituo viwili kwakufuatisha vipande vifupivifupi
                  ulivyovigawa katika mstari, na weka alama kwenye uzi huo
                  kuelekea upande wa pili. Funga fundo la pili kwenye uzi





                                                 65



                                                                                          31/10/2024   19:19
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   65
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   65                                           31/10/2024   19:19
   67   68   69   70   71   72   73   74   75   76   77