Page 77 - Jiografia_Mazingira
P. 77

Maswali

            1.  Tumia uzi kukokotoa umbali wa kutoka Kilimani hadi Hekima.

            2.  Tumia kipande cha karatasi kukokotoa urefu wa reli.

        FOR ONLINE READING ONLY
            3.  Tumia bikari kukokotoa urefu wa mto Bariadi kutoka katika
               kilele cha mlima hadi Ziwa Gagadi.


          Kupima umbali kidijitali

          Pamoja na kubaini umbali wa vitu vilivyonyooka na visivyonyooka
          kwa kutumia njia za kawaida, pia tunaweza kubaini umbali kwenye

          ramani kwa kutumia njia za kidijitali. Hatua zifuatazo zinaeleza
          namna ya kutumia programu ya “Google My Maps” kupima umbali:

             (a) Tumia kompyuta au simujanja kufungua tovuti ya Google,
                kisha tafuta “Google My Maps” na bofya “My Maps” kama

                inavyoonekana kwenye Kielelezo namba 21.

























                 Kielelezo namba 21: Kufungua programu ya Google My Maps

             (b) Baada ya kufungua “Google My Maps”, tafuta eneo unalotaka
                kupima umbali kati ya vituo viwili.  Kwa mfano, tutatafuta
                Munguri FDC kama inavyoonekana kwenye Kilelezo namba

                22 ili kupima umbali kati ya Munguri FDC na shule ya msingi
                Munguri.




                                                 70



                                                                                          31/10/2024   19:19
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   70
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   70                                           31/10/2024   19:19
   72   73   74   75   76   77   78   79   80   81   82