Page 73 - Jiografia_Mazingira
P. 73

pale kilipoishia kituo B kama inavyoonekana katika Kielelezo
                  namba 14.






        FOR ONLINE READING ONLY








              Kielelezo namba 14:  Kufuatisha mstari kwa uzi kutoka kituo A hadi kituo B


              (c) Tumia skeli ya mstari kubadili umbali wa kwenye ramani
                  kwenda umbali halisi kwenye ardhi kwa kufanya yafuatayo;

                  (i) Nyoosha uzi na ulaze katika skeli ya mstari, hakikisha

                     fundo la kwanza linalala kwenye sifuri (0) na fundo la pili
                     upande wa kulia wa skeli ya mstari;

                  (ii) Ikiwa fundo la pili lipo sambamba na namba fulani kwenye
                     skeli ya mstari, namba hiyo inawakilisha umbali halisi katika
                     ardhi kati ya vituo viwili;

                  (iii)  Ikiwa fundo la pili liko katikati ya namba mbili, nakili

                     namba ya kushoto na weka alama nyekundu kwenye uzi
                     kama inavyoonekana katika Kielelezo namba 15. Kwa
                     mfano, namba ya kushoto iliyonakiliwa kwenye Kielelezo
                     namba 15 ni Km 1. Kisha, hamisha uzi kwenda kushoto

                     hadi kufikia fundo la pili liwe sambamba na sifuri (0) na
                     alama nyekundu iliyowekwa iwe upande wa kushoto wa
                     skeli ya mstari;

                  (iv)  Mwisho, nakili namba iliyopo kwenye skeli ya mstari pale
                     ilipoishia alama nyekundu ya kwenye uzi. Kwa mfano, meta
                     500 imenakiliwa kama inavyoonekana katika Kielelezo

                     namba 15. Hivyo, umbali wa ardhi kati ya pointi A na B ni
                     Kilometa 1 na meta 500.






                                                 66



                                                                                          31/10/2024   19:19
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   66                                           31/10/2024   19:19
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   66
   68   69   70   71   72   73   74   75   76   77   78