Page 106 - SayansiStd4
P. 106

Hatua
              1.  Chukua  bakuli  angavu  lililo  tupu au bika.  Tumbukiza

                    sehemu ya penseli ndani ya bakuli hilo ukiwa umeishikilia.

              2.  Chunguza jinsi penseli inavyoonekana.
          FOR ONLINE READING ONLY

              3.  Mimina  maji  kutoka  kwenye  jagi  mpaka  yafike  nusu  ya
                    bakuli au bika kama inavyoonekana  kwenye Kielelezo
                    namba 12.


              4.  Chunguza tena mwonekano wa penseli iliyopo ndani ya
                    bakuli  au  bika  baada  ya kuweka  maji. Je, kuna  tofauti
                    gani kwenye mwonekano wa penseli kabla na baada ya
                    kumimina maji?


              Matokeo
              Penseli inaonekana imepinda kutokana na miale ya mwanga

              kupinda

              Hitimisho

              Jaribio  linathibitisha kwamba  miale  ya mwanga  hupinda

              inapopita kwenye midia angavu tofauti.

              Matumizi ya nishati ya mwanga

              Mwanga        hutumika       katika     mambo        mbalimbali       kama
              inavyooneshwa kwenye Jedwali namba 4.

              Jedwali namba 4: Matumizi ya nishati ya mwanga



               Picha                                 Maelekezo

                                                     Kuona: Mwanga hutusaidia

                                                     kuona vitu.  Bila mwanga,
                                                     hatungeweza  kuona rangi,
                                                     maumbo, au vitu vilivyo karibu
                                                     nasi.



                                                   99




                                                                                            14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   99
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   99                                   14/01/2025   18:39
   101   102   103   104   105   106   107   108   109   110   111