Page 109 - SayansiStd4
P. 109

Sauti inapotengenezwa,  chembe za hewa hutetema na
              kugongana. Hali hii, husababisha  mitetemo ambayo hutoa
              mawimbi ya sauti. Tunaweza kusema kuwa mawimbi ya sauti
              husambaa  kwa  mitetemo  ya  vitu.  Vitu  hivi  husafirisha  sauti
          FOR ONLINE READING ONLY
              kwa kutetemesha chembechembe. Kwa  mfano,  ndege ya
              abiria inaweza kuwa  mbali angani, lakini sauti husikika kwa
              kutetemesha molekuli za hewa kutoka kwenye ndege kwenda
              sikioni. Sauti inasafirishwa kutoka kwenye ndege hadi kwenye

              sikio kupitia hewa.

              Kuakisiwa kwa sauti

              Sauti iliyoakisiwa huitwa mwangwi. Mwangwi hutokea wakati
              mawimbi ya sauti yanapogonga kutoka kwenye uso wa vitu na

              kurudi kwa msikilizaji. Hali hii hutokea sehemu ambazo mawimbi
              ya sauti hukutana na vitu vinavyoakisi sauti.  Mfano wa vitu
              vinavyoakisi sauti ni ukuta au vitu vikubwa. Muda ambao sauti

              huchukua mpaka kurudi kwa msikilizaji husaidia kupata umbali
              wa kiliko kitu kilichoakisi.



               Kazi ya kufanya namba 7


              Kufanya kitendo cha kutoa mwangwi

              1.  Ingia kwenye ukumbi usio na kitu, kisha simama angalau
                    umbali wa mita 17 kutoka kwenye moja ya ukuta kama
                    Kielelezo namba 14 kinavyoonesha.


              2.  Ita kwa sauti kubwa. Je, unasikia nini?


              3.  Andika matokeo ya kitendo ulichofanya.














                                                   102



                                                                                            14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   102
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   102                                  14/01/2025   18:39
   104   105   106   107   108   109   110   111   112   113   114