Page 114 - SayansiStd4
P. 114
Uhusiano kati ya nishati mbalimbali
Nishati ya umeme inaweza kubadilishwa kutoka nishati moja
kwenda nyingine kutegemeana na kifaa kilichotumika. Kwa
mfano, glopu katika kurunzi hubadilisha nishati ya umeme
FOR ONLINE READING ONLY
kutoka kwenye selikavu na kutoa nishati ya mwanga na joto.
Chunguza kwa makini matendo yanayofanyika katika Kielelezo
namba 18, kisha fanya kazi namba 11.
(a) (b) (c)
Kielelezo namba 18: Matumizi ya nishati ya mwanga, sauti na joto
Kazi ya kufanya namba 11
Kuchunguza aina za nishati katika mazingira na uhusiano
wake.
Tumia maktaba, matini mtandao au vyanzo vingine vya taarifa
kufanya yafuatayo:
1. Orodhesha aina za nishati zinazoonekana katika
Kielelezo namba 18 (a), 18 (b) na 18 (c).
2. Bainisha uhusiano wa nishati zinazoonekana katika
Kielelezo namba 18 (a), 18 (b) na 18 (c).
107
14/01/2025 18:39
SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd 107
SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd 107 14/01/2025 18:39