Page 57 - SayansiStd4
P. 57

Sura ya Tatu






                                                Maada
          FOR ONLINE READING ONLY




                Utangulizi

                Mazingira yanahusisha vitu vyenye uzito na vinavyochukua
                nafasi. Vitu hivyo huitwa maada. Katika sura hii, utajifunza

                hali za maada. Pia, utafanya majaribio sahili ya kuchunguza
                hali zake. Umahiri  utakaoujenga  utakuwezesha kutumia
                maada mbalimbali katika maisha ya kila siku.






                                      Kuhusu vitu mbalimbali vyenye uzito
                             Fikiri
                                      na vinavyochukua nafasi





              Dhana ya maada

              Maada ni kitu chochote chenye uzito na kinachochukua nafasi.

              Mfano wa maada ni kama vile jiwe, maji na hewa.



                Kazi ya kufanya namba 1



               1.  Tumia maktaba, matini mtandao  au vyanzo vingine
                     kutafuta taarifa kuhusu dhana ya maada. kisha toa
                     mifano mingine ya maada.


               2.  Kusanya vitu mbalimbali, chunguza sifa zake, na uviweke
                     kwenye makundi kulingana na hali za maada kama vile
                     yabisi, kimiminika na gesi.




                                                   50



                                                                                            14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   50
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   50                                   14/01/2025   18:39
   52   53   54   55   56   57   58   59   60   61   62