Page 58 - SayansiStd4
P. 58

Hali za maada

              Zipo hali mbalimbali za maada. Katika sehemu hii utajifunza
              hali tatu za maada ambazo ni yabisi, kimiminika na gesi.

          FOR ONLINE READING ONLY
              Yabisi

              Aina hii ya maada huwa imara na ngumu.  Yabisi ina umbo
              maalumu. Mawe, sufuria na kuni ni mifano ya vitu  yabisi.
              Kielelezo namba 1 kinaonesha mifano ya vitu yabisi.
















                              Mawe                               Sufuria                        Kuni
                               Kielelezo namba 1: Mifano ya vitu yabisi

              Kimiminika

              Kimiminika  hakina  umbo maalumu
              bali huendana na kifaa au chombo

              kilimowekwa. Ukimimina maji kwenye
              kifaa, maji  yanachukua  nafasi  na
              kuendana  na umbo  la kifaa hicho.
              Mifano       mingine       ya      kimiminika
              inahusisha  vitu mbalimbali  ikiwemo

              maji, juisi  na soda. Kielelezo  namba
              2 kinaonesha kimiminika kikimiminwa
              kwenye glasi.

                                                       Kielelezo namba 2: Kimiminika
                                                          kikimiminwa kwenye glasi







                                                   51




                                                                                            14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   51
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   51                                   14/01/2025   18:39
   53   54   55   56   57   58   59   60   61   62   63